Wednesday, September 5, 2012

KUTOA NI MOYO





Nikikata utepe na Paschal Cassian kwa ajili ya uzinduzi
Paschal akiwa jukwaani anatumbuiza mashabiki


Martha Mwaipaja naye alitoa mchango wake jukwaani


Nilipata fursa ya kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa album mpya ya Injili ya Paschal Cassian (Mshindi wa BSS 2009) iitwayo 'Yasamehe Bure' katika hafla iliyofanyika Jumapili iliyopita. Paschal alichagua kufanya uzinduzi huo Uwanja wa Fisi, Manzese kwa nia ya kuchangisha kiasi cha millioni 30 kupitia mauzo ya album hiyo kwa ajili ya kupambana na biashara ya ukahaba inayofanywa na wasichana wa eneo hilo.

Bila kumuangusha, nami nilitoa mchango wangu ili kusaidia kufanikisha kampeni hiyo muhimu. Binafsi naamini kuwa, ili kupambana na biashara hiyo haramu inatakiwa kwanza wanaume waepukane na tabia ya kununua wasichana hao kwa kuwa wanunuzi wasipokuwepo basi hata wauzaji hawatakuwepo. 

No comments:

Post a Comment