Tuesday, November 6, 2012

WAZO LA LEO

Mpaka sasa nani unahisi atanyakuwa kitita cha milioni 50? Kumbuka kumpigia kura mshiriki umpendae mara nyingi uwezavyo...... Jumanne nje!


Thursday, October 25, 2012

WAZO LA LEO



"Kila jambo tunalokumbana nalo katika maisha, hata kama ni baya vipi, jambo hilo linatokea katika maisha yetu kutufunza kitu." - Iyanla Vanzant

Wednesday, October 24, 2012

WAZO LA LEO


"Mtu akikuonyesha yeye ni nani, muamini mara hiyo ya kwanza" - Maya Angelou

Monday, October 15, 2012

MUONEKANO WANGU KATIKA MAJARIDA TOFAUTI

Pata fursa ya kuangalia muonekano wangu katika majarida tofauti niliyowahi kufanya nao mahojiano.








WAZO LA LEO

"Hamna mtu atakayekupenda zaidi ya unavyojipenda wewe mwenyewe"

Friday, October 5, 2012

WAZO LA LEO

"Kama hupendi kitu, badilisha. Kama hutofanikiwa kukibadilisha, badilisha mtazamo wako. Si kulalamika." – Maya Angelou

Tuesday, October 2, 2012

KANGA NA MAANDISHI YAKE

Maandishi ya kanga huwa yananifurahisha sana. Kama Mtanzania, najivunia sana utamaduni huu na muendelezo wa kudumisha utamaduni wetu wa kuvaa kanga.

Kwa mtazamo wangu, maandishi ya kanga yanafundisha namna moja au nyingine, ukiyasoma kwa kina na kupata kuelewa kanga hiyo imebeba ujumbe gani.

SIRI NI YA WAWILI

UTAUMIZA ROHO YAKO

USIMLAUMU SISIMIZI SUKARI HAIMALIZI
Mbali na kuwa maandishi mengi ya kanga ni misemo ya Kiswahili, pia maandishi hayo yanaweza yakawa ni  ujumbe wa upendo, tahadhari, onyo au tu mtu binafsi kapenda kueleza anachohisi moyoni.