Friday, September 28, 2012
WAZO LA LEO
''Mtu anayesema kitu fulani hakiwezekani, asimuingilie ama kumpinga yule ambaye anaweza kukifanya'' Unknown.
Wednesday, September 26, 2012
UZINDUZI WA EBSS HOUSE
Hafla ndogo ilifanyika kwa ajili ya kuzindua EBSS HOUSE. Washiriki 12 bora waliochaguliwa watapata fursa ya kuishi ndani ya nyumba hii hadi hapo mshindi atapo patikana.
WAZO LA LEO
Hebu jiulize,
''Ni kitu gani kikubwa wewe ungejaribu kama ungejua kuwa huwezi kushindwa? - Robert H. Schuller''
''Ni kitu gani kikubwa wewe ungejaribu kama ungejua kuwa huwezi kushindwa? - Robert H. Schuller''
Monday, September 24, 2012
TAMADUNI ZA WENZETU
Wanawake wa kabila la Himba lililoko nchini Zambia wanajipaka matope wanayo yaita 'Otjize' na ni kwasababu hiyo wamepewa jina la 'Red Women.'
Inasemekana matope hayo wanayapaka ili kuzuia wadudu na jua lakini wahimba wenyewe wanasema wanasababu zao muhimu zinazowafanya wapake matope hayo.
Matope haya yanapakwa na wanawake wa Himba kila waamkapo asubuhi lakini wanaume hawaruhusiwi kupaka.
Thursday, September 20, 2012
BEHING THE SCENE
Nikiwa napambwa na Miss Ria. Huyu mwanadada ni mtaalam wa urembo ambaye pia anawapamba washiriki wa EBSS 2012 na kuhakikisha wamependeza........
Hii ni behind the scene kabla filming ya EBSS haijaanza.
Hii ni behind the scene kabla filming ya EBSS haijaanza.
WASHIRIKI WA EBSS WAONYESHA VIPAJI VYAO
EBSS tunawakaribisha wadau wetu wote kuangalia BURE, LIVE perfomance ya Top 20 inayofanyika leo, Budget Hotel njia panda ya Bahari Beach, Kunduchi. Muda ni Saa 7:00 mchana!
KARIBUNI SANA!!!
KARIBUNI SANA!!!
Tuesday, September 18, 2012
NIKIONGELEA KUHUSU BSS
Nilipata fursa ya kuhojiwa na jarida la Bang Magazine. Mazungumzo yetu yalihusisha masuala yote kuhusiana na Bongo Star Search......
Kwa wale wote wenye maswali kuhusiana na EBSS, majibu mtayapata kwenye mahojiano baina yangu na Bang Magazine. Jarida hili linatarajia kuwa mtaani hivi karibuni...... Usikose kununua!
Kwa wale wote wenye maswali kuhusiana na EBSS, majibu mtayapata kwenye mahojiano baina yangu na Bang Magazine. Jarida hili linatarajia kuwa mtaani hivi karibuni...... Usikose kununua!
Monday, September 17, 2012
WANAWAKE NA SIASA
Miaka ya hivi karibuni, wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika medani za siasa barani Afrika na hata wengine wakiwa wameshikilia wadha mkubwa serikalini.
Hawa ndio baadhi ya wanawake wenye nguvu kisiasa Afrika.
Hawa ndio baadhi ya wanawake wenye nguvu kisiasa Afrika.
Ellen Johnson Sirleaf - Rais wa Liberia |
Joyce Banda - Rais wa Malawi |
Ngozi Okonjo-Iweala - Waziri wa Fedha, Nigeria |
Luisa Dias Diogo - Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, Mozambique |
Anna Makinda - Spika wa Bunge, Tanzania Ni umahiri wa wanawake hawa ndio unaotupa nguvu sisi kama wanawake na kutuongezea kujiamini. |
WAZO LA LEO
"Kosa kubwa unaweza kufanya katika maisha ni daima kuogopa kwamba utafanya kosa." - Elbert Hubbard
Friday, September 14, 2012
Wednesday, September 12, 2012
EBSS EXCLUSIVE NDANI YA BAABKUBWA
Exclusive: EPIC BONGO STAR SEARCH....HUKU MAMBO NI MOTOO!
Baabkubwa Magazine toleo jipya linatarajia kutoka wiki hii likiwa na muonekano mpya huku ndani likiwa na line ya Zantel ambayo ina mkwanja na pia itakuwezesha kukupa nafasi ya kushindani zawadi kibao kutoka Zantel... Usikose kusoma toleo hili likiwa na habari mbalimbali kuhusiana na EBSS.
Baabkubwa Magazine toleo jipya linatarajia kutoka wiki hii likiwa na muonekano mpya huku ndani likiwa na line ya Zantel ambayo ina mkwanja na pia itakuwezesha kukupa nafasi ya kushindani zawadi kibao kutoka Zantel... Usikose kusoma toleo hili likiwa na habari mbalimbali kuhusiana na EBSS.
Tuesday, September 11, 2012
KIVUTIO
Umeshapigia kura?
Mlima Kilimanjaro ni miongoni mwa vivutio kutoka Tanzania ambavyo vimeingizwa kwenye shindano la kutafuta Maajabu Saba Asilia ya Afrika (SEVEN NATURAL WONDERS OF AFRICA). Vivutio vingine kutoka nchini ambavyo pia vimetajwa kwenye shindano hilo ni pamoja na Ngorongoro Crater na Serengeti National Park.
Mlima Kilimanjaro ni miongoni mwa vivutio kutoka Tanzania ambavyo vimeingizwa kwenye shindano la kutafuta Maajabu Saba Asilia ya Afrika (SEVEN NATURAL WONDERS OF AFRICA). Vivutio vingine kutoka nchini ambavyo pia vimetajwa kwenye shindano hilo ni pamoja na Ngorongoro Crater na Serengeti National Park.
Friday, September 7, 2012
WAZO LA LEO
"Ili kuwepo na maendeleo ya ukweli na haswa yanayo onekana, ni lazima wananchi washirikishwe - Julius Kambarage Nyerere''
Wednesday, September 5, 2012
KUTOA NI MOYO
Nikikata utepe na Paschal Cassian kwa ajili ya uzinduzi |
Paschal akiwa jukwaani anatumbuiza mashabiki |
Martha Mwaipaja naye alitoa mchango wake jukwaani |
Nilipata fursa ya kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa album mpya ya Injili ya Paschal Cassian (Mshindi wa BSS 2009) iitwayo 'Yasamehe Bure' katika hafla iliyofanyika Jumapili iliyopita. Paschal alichagua kufanya uzinduzi huo Uwanja wa Fisi, Manzese kwa nia ya kuchangisha kiasi cha millioni 30 kupitia mauzo ya album hiyo kwa ajili ya kupambana na biashara ya ukahaba inayofanywa na wasichana wa eneo hilo.
Bila kumuangusha, nami nilitoa mchango wangu ili kusaidia kufanikisha kampeni hiyo muhimu. Binafsi naamini kuwa, ili kupambana na biashara hiyo haramu inatakiwa kwanza wanaume waepukane na tabia ya kununua wasichana hao kwa kuwa wanunuzi wasipokuwepo basi hata wauzaji hawatakuwepo.
Subscribe to:
Posts (Atom)