Maandishi ya kanga huwa yananifurahisha sana. Kama Mtanzania, najivunia sana utamaduni huu na muendelezo wa kudumisha utamaduni wetu wa kuvaa kanga.
Kwa mtazamo wangu, maandishi ya kanga yanafundisha namna moja au nyingine, ukiyasoma kwa kina na kupata kuelewa kanga hiyo imebeba ujumbe gani.
|
SIRI NI YA WAWILI |
|
UTAUMIZA ROHO YAKO |
|
USIMLAUMU SISIMIZI SUKARI HAIMALIZI |
Mbali na kuwa maandishi mengi ya kanga ni misemo ya Kiswahili, pia maandishi hayo yanaweza yakawa ni ujumbe wa upendo, tahadhari, onyo au tu mtu binafsi kapenda kueleza anachohisi moyoni.
No comments:
Post a Comment